KUTOKANA na
presha ya usalama kuwa mdogo wakati wa mechi ya watani wa jadi, Simba na
Yanga, Bodi ya Ligi imeamua kuongeza askari wa usalama hadi 400 kwa
ajili ya kulinda amani siku watani hao watakapokutana.
Hayo yamesemwa na ofisa mtendaji wa bodi
hiyo, Silas Mwakibinga, ambaye amesema kuwa wameamua kuongeza idadi ya
askari hadi kufikia 400 ambao watakuwa na vitendea kazi kama farasi na
mabomu ya machozi kutokana na vitendo vya fujo ambavyo vimekuwa
vikijitokeza katika mechi za watani.
Kocha Mzambia, Patrick Phiri.
Simba kwa sasa ipo chini ya kocha Mzambia, Patrick Phiri huku Yanga ikiwa chini ya Mbrazil, Marcio Maximo.
“Tanzania hatujafikia hatua ya kufungia mashabiki.
Kwanza fujo za mashabiki wetu si za kuhatarisha maisha ya wachezaji
kama nchi nyingine, mfano Misri, pili ‘nature’ ya mpira wetu ni wa
kutegemea viingilio, hivyo tumeamua kuboresha sekta ya ulinzi msimu huu
kwenye mechi kubwa,” alisema Mwakibinga katika mahojiano maalum na
Championi Jumatatu.
Kocha Mzambia, Patrick Phiri.
No comments:
Post a Comment