Monday, 28 July 2014

Boko Haram wazilenga Nigeria na Cameroon



Boko_haram

 Read More
Kundi la wapiganaji wa Kiislam la Boko linatuhumiwa kuendesha mapigano kaskazini mwa Nigeria na katika mpaka wa Nigeria na Cameroon.
Maofisa wa polisi nchini Cameroon wamesema kuwa ndege za kivita na vikosi vya kijeshi vimepelekwa karibu na mpaka wa Cameroon baada ya tukio la kutekwa kwa mke wa mwanasiasa maarufu ambaye pia ni naibu waziri mkuu Amadou Ali
Kiongozi mwingine wa kidini Seini Boukar Lamine anadaiwa kutekwa na wapiganaji hao wa Boko Haram huku mapigano yakiripotiwa kuendelea katika eneo hilo.
Katika mji wa kaskazini mwa mji wa Kano imearifiwa kuwa wane wameuawa katika milipuko miwili inayodaiwa kutekelezwa na kundi la Boko Haram.
Sherehe za kukamilisha mfungo wa Ramadhan zimefutwa kaskazini mwa Nigeria mwaka huu kutokana na hofu ya usalama.

No comments:

Post a Comment