Tuesday, 14 October 2014

DENTI AJICHOMA KISU KISA MAPENZI


LOO! Mwanafunzi wa Chuo cha T.I.A tawi la mkoani Singida, Moza Kasim Mohemed (20) ambaye ni mkazi wa jijini Dar es Salaam, amejichoma kisu tumboni kwa madai ya kuchoshwa na usaliti wa mpenzi wake aitwaye Joel ambaye pia ni mwanafunzi wa chuo hicho.

Moza Kasim Mohemed akiwa hoi baada ya kujichoma kisu cha tumbo.
Tukio hilo la kushangaza lilitokea usiku wa kuamkia Oktoba 10, mwaka huu maeneo ya Jovena katika Hosteli za Miami ambapo Moza alikuwa akiishi na mpenzi wake huyo.
Chanzo chetu kilidai kuwa, siku hiyo muda mfupi kabla ya tukio hilo kulitokea kutoelewana kwa wawili hao ambapo majirani walimsikia Joel akimtuhumu Moza kwamba amekuwa msaliti na anahisi ana simu nyingine ya ziada ambayo anaitumia yeye akiwa hayupo.
Muonekano wa kisu hicho baada ya kujichoma.
Timbwili lilisikika kwa muda mrefu kiasi kwamba ilibidi majirani waanze kuchungulia dirishani na wakamsikia Moza akimwambia Joel kwamba, kwa vile hamwamini hadi anafikia kumpiga bora ajichome kisu afie mbali.Kwa mujibu wa chanzo chetu, Joel naye alisikika akimjibu Moza kwa kumwambia kama dhamira yake ni hiyo, basi ajichome tu.Akiwa hospitalini baada ya kutolewa kisu tumboni.
Malumbano hayo yaliendelea kuchukua ukurasa mpya ambapo Joel aliendelea kumpa kibano na baadaye alimuacha na kutoka nje, baada ya dakika chache zikasikika kelele za ajabu kutoka kwa Moza ambapo majirani ambao ni baadhi ya wanafunzi wenzake wakatoka na kuingia chumbani na kumkuta akigalagala na damu zikimvuja huku kisu kikiwa tumboni.
“Hawa watu walikuwa na tabia ya kukwaruzana mara kwa mara na Joel alikuwa akimpiga yanaisha ila siku hiyo ilikuwa ni mzozo wa hatari, baada ya tukio watu walijaa lakini kila mtu akawa anaogopa kumgusa Moza, Joel alipata ujasiri yeye na rafiki yake wakambeba na kumkimbiza Hospitali ya Mkoa wa Singida,” kilisema chanzo.
Hostel aliyokuwa anaishii Moza Kasim Mohemed .
Kikaendelea: “Jana (juzi Jumapili) tulikwenda hospitali kumsalimia, tulikuta ameshatolewa kisu na ameshashonwa, hali yake inaendelea vizuri, ila habari ya mjini Singida kwa sasa ni juu ya tukio hilo, hata tulipofika hospitali tulikuta wanafunzi wengi.”

No comments:

Post a Comment