Friday, 17 October 2014

HUKUMU YA PISTORIUS YAINGIA SIKU YA NNE

Mwanariadha wa Afrika Kusini Oscar Pistorius (kulia) akitembea ndani ya mahakama. Mwanariadha wa Afrika Kusini Oscar Pistorius anatakiwa kupewa 'adhabu ya kali' kwa kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp, binamu yake Steenkamp ameliambia jopo la mahakama inayosikiliza hukumu yake mjini Pretoria.

Kim Martin ameiambia mahakama kuwa Pistorius "anahitajika kulipa kwa kile alichotenda."
Upande wa mashitaka unajenga hoja kwamba Pistorius mwenye umri wa miaka 27 ahukumiwe kifungo jela.
Mwanariadha wa Afrika Kusini Oscar Pistorius (aliyesimama) akiongea na mwanasheria wake, Barry Roux.
Mwezi uliopita , alipatikana na hatia ya kumuua mpenziwe bila kukusudia lakini aliondolewa mashitaka ya kuua na kwa kosa la sasa adhabu yake hufikia miaka 15 kifungo jela, lakini jaji anaweza kubatilisha au kumtoza faini.
Upande wa utetezi umekuwa upendekeza kuwa Pistorius atumikie adhabu ya kifungo cha nyumbani na kufanya kazi za kijamii kwa kosa hilo- pendekezo ambalo limetajwa na mwendesha mashitaka Gerrie Nel kuwa "si sahihi na linatisha".
Upande wa mashitakam umesisitiza kuwa Pistorius lazima afungwe jela, wakisema vitendo vyake vya kizembe vimesababisha "familia kupata pigo kubwa".
Oscar Pistorius akitembea ndani ya mahakama.
'Hatulipizi kisasi'

Katika kikao cha kusikiliza mwenendo wa hukumu hiyo, Bi Martin amesema ana hofu na Pistorius.

"Familia yangu si ya watu wanaOtaka kulipiza kisasi, tunahisi kwamba kumpiga mtu risasi nyuma ya mlango ambaye tena hana silaha, unahitaji adhabu ya kutosha, amesema.

Jumatano, Bi Martin alielezea kuumizwa kwake aliposikia mwanamitindo huyo wa Afrika Kusini mwenye umri wa miaka 29 aliuawa kwa kupigwa risasi, akisema kifo chake "ulikuwa mwisho wa dunia".

No comments:

Post a Comment