Tuesday, 30 September 2014

KIGWEMA, BEST NASSO: TUTAKUKUMBUKA SIDE BOY


Wasanii Best Nasso kushoto, Hamisi Kibiti ambaye ni Meneja wa Best Nasso na kulia ni msanii Kigwema kwenye picha ya pamoja wakiwa safarini kuelekea Lindi kwenye mazishi ya msanii mwenzao.

KABURI LA RECHO LALOA MACHOZI!


Roho inauma! Kwa mara nyingine, kaburi la aliyekuwa staa wa sinema za Kibongo, Rachel Leo Haule ‘Recho’ (pichani) limeloa machozi ya mastaa wakati wa kusimikwa msalaba baada ya kujengwa na kuonekana la kisasa, Ijumaa Wikienda lilikuwepo.

MILIONEA WA JWTZ ALIVYOUAWA KWA RISASI



NI taharuki iliyojaa majonzi na simanzi kufuatia Jeshi la Wananchi wa Tanzania ‘JWTZ’ Kikosi cha CMTU jijini Dar kuondokewa na mpiganaji wake, Sajenti Yohana  Lugendo Gweso (40) ambaye alikuwa milionea aliyepigwa risasi sita mwilini na kufariki dunia papo hapo.

PAKA AFUGWA HIRIZI MTINI


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, paka mwenye hirizi kubwa shingoni akiwa hai alikutwa amepigiliwa misumari juu ya mti uliopo jirani na Msikiti wa kwa Mtawara uliopo Kata ya Mwembesongo mkoani hapa.

NILISHUHUDIA NIKICHOMWA MOTO


MTU mmoja aliyefahamika kwa jina la Richard Osward (40) mkazi wa Tabata Segerea, hivi karibuni alinusurika kuuawa kwa kuchomwa moto na wananchi baada ya kuhisiwa kuwa mwizi alipokutwa alfajiri akiwa na mfuko ambao ndani yake kulikuwa na bomba, huko Segerea.

SEREMALA AJINYONGA, AACHA MASWALI


KATIKA hali ya kushangaza, mtu mmoja ambaye ni fundi seremala aitwaye Emmanuel Carlos, mkazi wa Kwabinyau Magomeni jijini Dar amekutwa akiwa amejinyonga saa mbili asubuhi Septemba 23, mwaka huu katika kile kinachodaiwa kuchoshwa na mgogoro wa kifamilia.

Monday, 29 September 2014

BONDIA WA KIKE MWAFRIKA ACHUKUA UBINGWA WA NGUMI ULAYA


Bintou Schmill a.k.a 'The Voice' baada ya kumchapa Mirjana Vujic kwa K.O.

AJALI YATOKEA BARABARA YA MOSHI - ARUSHA MCHANA HUU




Polisi wa usalama barabarani akiliangalia kwa karibu moja ya gari lililoharibika vibaya katika ajali iliyotokea mchan huu katika eneo la Sadal njia ya Moashi - Arusha.

MSANII WA BONGO FLEVA SIDE MNYAMWEZI AFARIKI DUNIA




Muimbaji wa muziki wa Bongo Fleva Said Salim 'Side Boy Mnyamwezi' enzi za uhai wake.

Friday, 26 September 2014

NI SHEEDA! MUIGIZAJI WA FILAMU SLIM ADAIWA KUGOMA KUREJESHA GARI

Sto
NI sheeda! Muigizaji wa filamu za Kibongo, Salim Omary ‘Slim’ amejikuta akiwekwa nguvuni katika Kituo cha Polisi cha Makangarawe, Yombo-Buza, jijini Dar akidaiwa kugoma kurejesha gari aina ya Land Lover Discovery walilopewa zawadi siku ya ndoa.
Muigizaji wa filamu za Kibongo, Salim Omary ‘Slim’.
Gari hilo walipewa na wakwe zake alipofunga ndoa na binti yao aitwaye Asia Morgan, mwaka jana lakini ilipofika Mei mwaka huu (takriban miezi tisa tu ndani ya ndoa), wawili hao walitengana na kusababisha wakwe hao wageuke mbogo kudai chao kwa maelezo kwamba walitoa zawadi hiyo kwa binti yao hivyo kwa kuwa wametengana, wanataka chao.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, Asia alifikia uamuzi wa kwenda kuishi nyumbani kwao Tegeta, jijini Dar baada ya kushindwa kuvumilia tabia ya wivu wa kupindukia aliyokuwa nayo Slim.
“Baada ya kutengana wazazi wa msichana huyo walimwambia Slim awakabidhi gari moja kwa kuwa anayo mawili na kama anataka Discovery (Land Lover) wamuachie lakini wapate moja kwa ajili ya binti yao kuendea chuo,” kilisema chanzo.
Salim Omary ‘Slim’ akiwa na aliyekuwa mke wake.
Akizungumza kwa jazba, mama mzazi wa Asia alisema, walimzawadia gari hilo kwa kuwa wote walikuwa wanapenda tasnia ya filamu hivyo gari hilo lingemsaidia yeye na mume wake katika shughuli zao.
“Kinachouma ni kwamba tusingefikishana hapa lakini tulishamuomba sana Slim kurudisha gari hilo au ampe mwanetu gari lingine abaki na hilo kama analipenda lakini alikataa na mbaya zaidi ana kila kitu, kuanzia ufunguo na kadi ya gari kitu ambacho hatendi haki kwa mtoto wetu,” alisema mzazi huyo.
kizidi kutema cheche mbele ya kinasa sauti cha Ijumaa, mzazi huyo alisema licha ya Slim kwenda Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) kushtaki ili arudiane na binti yao, haitawezekana.
“Nashindwa kuelewa kabisa jambo hili nilijitahidi sana kulivumilia lakini nimeona imeshindikana kabisa hivyo tuliamua kwenda nyumbani na kumchukua kumfikisha kituoni hapa maana sisi tulimfanya kama mtoto wetu lakini yeye amekuwa mkaidi,” alisema mama huyo.
Salim Omary ‘Slim’akiwa katika kituo cha polisi Makangarawe, Yombo-Buza.
Mwandishi wetu alimfuata Slim kituoni hapo na kuzungumza naye kuhusiana na sakata hilo ambapo alisema anachofahamu yeye ni kwamba zawadi inapotolewa kwenye harusi na wazazi inakuwa ni ya mke na mume lakini anawashangaa wazazi hao kuidai ikiwa hata mkewe hajampa talaka.
“Nashindwa kuelewa kabisa kwa sababu wazazi wa mke wangu walitoa gari lile kama zawadi sasa sielewi kwa nini walidai tena wakati mke wangu sijamuacha, suala hili lipo Bakwata.
“Isitoshe, gari hilo nimelitengeneza sana mpaka kufikia lilivyo sasa kwani bado lipo gereji, lakini kwa kuwa wameamua kunidai, baada ya miezi mitatu nitakuwa nimewapa gari lao,” alisema Slim.

MATAJIRI WALIKUWA MASKINI, UNACHOSHINDWA WEWE NI KIPI?

Bill Gate.

MBINU KUMI ZA KUFUFUA PENZI LILILOKUFA-2

Namshukuru Mungu kwa kuniweka hai mpaka leo tunapokutana tena katika busati letu la mahaba, kuendelea kujadiliana kuhusu mada tuliyoianza wiki iliyopita ya mbinu za kufufua penzi lililokufa.

AMANDA AWA MBOGO BARABARANI


Msanii wa filamu, Tamrina Posh ‘Amanda’ hivi karibuni alizua balaa la aina yake baada ya kukatiza mtaani akiwa amevaa kigauni kilichokaribia kuacha wazi makalio yake.

MSIBA WAZIMA BWEBWE ZA AUNT MAREKANI



Staa wa filamu za Kibongo, Aunt Ezekiel amelazimika kusitisha bata alizokuwa akila nchini Marekani baada ya kupata msiba wa mdogo wake aliyefariki dunia juzikati.

LULU AWA BILIONNEA HATARI..!



Madai mazito ya kushtua mtaani yanasema kwamba staa wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, mambo yake kwa sasa yapo juu ya mstari baada ya bilionea kutoka jijini Arusha (jina tunalihifadhi kwa sasa) kudaiwa kujitosa kumlea akianza kwa kumpangishia jumba kubwa la kifahari.

MADEE ALIVYOSOTESHWA GEREZANI




Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva a.k.a Rais wa Manzese, Hamad Ally ‘Madee’ hivi karibuni alilala katika Kituo cha Polisi cha Kigamboni, Dar  akihusishwa na utekaji wa dereva wa bodaboda, Suedi Waziri (pichani) kisha kumpa kipigo ambapo inadaiwa alisoteshwa kinomanoma.

STEVE NYERERE AAIBIKA UWANJAWI




NYOTA wa kuigiza sauti za watu maarufu aliye pia mwigizaji wa sinema za Kibongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ wikiendi iliyopita alijikuta akiaibika kwa kuzomewa na kupopolewa kwa chupa za maji na mashabiki wa Klabu ya Simba baada ya kuingia uwanjani na demu aliyevaa ‘kihasarahasara’.

Hatima ya Qatar na kombe la dunia 2022

Aliyekua makamu wa Rais wa Fifa,Mohamed bin Hammam

MECHI YA SIMBA NA YANGA YAHAIRISHWA

     Mechi ya Yanga dhidi ya Simba (Picha na Erasto).

Thursday, 25 September 2014

Machester City yaiadhibu sheffield W

Wachezaji wa Manchester City

Suarez angojewa kwa hamu Barcelona


Luis Suarez

Waaga mchuano baada ya kuagizwa kuvua hijab

Timu ya wanawake ya Qatar ya mchezo wa mpira wa kikapu imejiondoa kutoka mashindo ya bara Asia

Asamoah Gyan akana madai ya kafara


Familia ya Gyan imeelezea kushangazwa na tetesi kuwa alimtoa kafara rafiki yake

Wafuasi wa Boko Haram wajisalimisha

Wanamgambo wa Boko Haram
Jeshi nchini Nigeria limesema zaidi ya wafuasi 260 wa Boko Haram wamejisalimisha Kaskazini mwa nchi hiyo.

Tetesi za iPhone 6 kujipinda

Wataalamu wana hisia mseto kuhusu ikiwa Apple inapaswa kujibu madai ya iPhone 6 kujipinda

Ahukumiwa kifo Kenya kwa kuavya mimba


Mahakama moja nchini Kenya imemhukumu muuguzi mmoja kunyongwa kwa kuavya mimba.

DIMPOZI,VANESSA MDEE SASA MAHABA NIUE

SIKU chache baada ya mkali wa Bongo Fleva, Omar Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ kuripotiwa kuwa anatembea na mwanamitindo Jokate Mwegelo, imedaiwa kuwa amemmwaga na kuhamishia ‘mahaba niue’ kwa mtoto mzuri anayefanya muziki wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee.

MADEE ATEKA MWENDESHA BODA BODA


Rais wa Manzese ambaye ni staa wa Bongo Fleva, Hamad Ally ‘Madee’ amelala nyumba ya nondo za mahabusu baada ya kutiwa mbaroni akihusishwa na utekaji wa dereva wa bodaboda, Suedi Waziri (pichani) kisha kumpa kipigo cha mbwa mwizi.

AFANDE SELE ANASWA NA DEMU MPYA




MKONGWE wa muziki wa kizazi kipya Seleman Msindi ‘Afande Sele’, juzikati alinaswa akiwa na demu mpya akiwa ni siku moja tu baada ya kufanyika kwa 40 ya aliyekuwa mzazi mwenzake, marehemu mama Tunda.

DIAMOND AMTOA MACHOZI MENNINAH


YALE madai kuwa sexy lady wa Bongo Fleva aliyeibukia kwenye Shindano la Kutafuta Vipaji la Epiq Bongo Star Search 2012, Meninah Abdulkareem ya kutaka kuolewa na staa wa muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ yamemtoa machozi mwanadada huyo.

Jaja atakiwa kuondoka nchini

KUFUATIA kutoa kipigo cha mabao 2-0 kwa timu ya Yanga, Klabu ya Mtibwa Sugar imesema kuwa straika wa Yanga, Mbrazili, Geilson Santos ‘Jaja’ atachemka katika ligi ya Bongo, na kusisitiza ni busara kama wangemuandalia mapema nyaraka zake ili arejee kwao kuendelea na majukumu mengine.

Wednesday, 24 September 2014

Kocha Mcameroon awapa Yanga ubingwa


KOCHA Mkuu wa Azam, Mcameroon, Joseph Omog, ameibuka na kuweka bayana sababu tatu ambazo zinaweza kuwagharimu katika harakati za kutetea ubingwa wao huku wakiushuhudia ukienda Jangwani au Msimbazi.

AJALI YA NOAH YAUA WAWILI MBEYA

Gari aina ya Toyota Noah lenye namba za usajili T162 BXM iliyopata ajali jana maeneo ya Igurusi mkoani Mbeya.

MWENDESHA BAJAJ AJERUHIWA KATIKA AJALI TEGETA

Dereva wa Bajaj iliyogongwa na Coaster eneo la Tegeta jana akiwa na majeraha mkononi.

UZINDUZI WA YA MOTO BAND WEMA AFANYA KUFURU.


“MADAM...Madam...Madam...” ndizo kelele zilizosikika wakati Beutiful Onyinye, Wema Sepetu ‘Madam’ alipokuwa akimtunza fedha nyingi dogo machachari wa Bendi ya Yamoto, Asilahi Isiyaka ‘Dogo Aslay’.

MKE AMBONDA HAWARA GESTI




Kila kukicha kunaibuka vituko vingi duniani, wamo wanaosema huenda ni mwisho wa dunia! Mama mmoja almaarufu kwa jina la Mama la Mama anadaiwa kumbonda hawara wa mumewe baada ya kumwekea mtego wa fumanizi kwenye nyumba ya kulala wageni (gesti).

MLELA AMPONDA NORA





KUFUATIA madai ya hivi karibuni ya mkongwe wa filamu Bongo, Nuru Nassoro ‘Nora’ kuwa baadhi ya waigizaji hawana sifa za kuwa wacheza sinema zaidi ya kuuza sura, msanii Yusuph Mlela amempa dongo zito akisema licha ya umri kuwa mkubwa, pia ana matatizo flani yanayomsumbua.

Tuesday, 23 September 2014

Obama aapa kuangamiza Islamic State

Rais Obama ameahidi kuangamiza Wanamgambo wa Islamic State 
Rais wa Marekani Barack Obama amesema Marekani itashambulia kundi linalojiitaa Islamic state kote nchini Syria na Iraq ili kuwanyima kabisa makao ya kujificha .

RAPPA T.I KUKAMUA BONGO



RAPPA kutoka nchini Marekani, Clifford Joseph Harris,'T.I' ni mmoja wa wanamuziki watakaopiga shoo katika Usiku wa Fiesta 2014 ndani ya Viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam.

DIAMOND YAMKUTA TENA UINGEREZA


Ni nuksi, gundu au hujuma? Ndivyo unavyoweza kujiuliza kufuatia tukio lingine baya lililomkuta staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa London nchini Uingereza ikiwa ni siku kadhaa tangu aliposababisha vurugu nchini Ujerumani, Ijumaa Wikienda lina ripoti kamili ya kilichojiri.

KIFO CHA MWALIMU BAADA YA MATESO- 2

Naendelea kuwaletea mambo yaliyojiri wakati Mwalimu Nyerere alipotoka kijijini kwake Mwitongo, Butiama kwenda kutibiwa nchini Uingereza hadi kifo chake.

MADHARA YA WANAFUNZI KUTOKUPENDA SHULE

Wanafunzi wengi wamekuwa na tabia ya kutokupenda shule. Wengi wao ukiwaliza kwa nini hutoroka masomo na kwenda kwenye makundi yasiyofaa hawajui msingi wake; pengine watakujibu kwa Kiswahili cha kisasa: “Shuleni kunaboa.” Yaani hakufurahishi.

BI. MOZA ATAMANI MWISHO UFIKE HARAKA


Soma hii! Kikongwe mmoja aliyefahamika kwa jina la Moza Nyanongwa (anakadiria ana miaka zaidi 100), mkazi wa Tandale, Kwatumbo jijini Dar amefunguka kuwa anatamani mwisho wa dunia ufike mapema kwa kudai kuchoshwa na mmomonyoko wa maadili unaoendelea nchini na dunia nzima kwa jumla.

MLIPUKO WAUA 12 CHINA



Taswira kutoka eneo la Kiwanda cha Nanyang ulipotokea mlipuko.
TAKRIBANI watu 12 wamefariki dunia huku 33 wakijeruhiwa katika mlipuko uliotokea jana katika kiwanda cha kutengeneza fataki jijini Liling katika Mkoa wa Hunan nchini China.

MKE WA KIGOGO MBARONI KWA WIZI WA MAGARI


Nuru Ramadhani Nasibu (pichani), mkazi wa jijini Dar es Salaam aliyekuwa akitafutwa na polisi wa nchini na wa kimataifa (Interpol) kwa kuhusishwa na wizi wa kuaminiwa wa magari matatu mali ya Dk. Emmanuel Matech  ametiwa mbaroni.

MWALIMU AKUTWA AMEFUNGWA MINYORORO KANISANI

Ndugu wa mtu anayedaiwa kuwa ni mlemavu wa akili, Galus Focus Nguruwe (35) ambaye ni mwalimu wa sekondari moja mjini Morogoro, wamelituhumu Kanisa la House of Prayer Shield of Faith Christian Fellowship lililopo Boko Magengeni jijini Dar kuwa wamemfunga mnyororo ndugu yao huyo kwa miezi nane mfululizo.

WACHUNGAJI MBARONI KWA ULAWITI WATOTO KANISANI


WATOTO sita, wakiwemo wawili wa kiume wenye umri wa miaka 8 hadi 14 wameharibiwa vibaya sehemu zao za siri baada ya kubakwa kanisani na watu wanaodaiwa ni wachungaji.

MTOTO ALIYEPANDA NDEGE BILA KUJULIKANA AANIKA UCHAWI WAZIWAZI


SAKATA la mtoto Happiness (10) aliyetikisa kwa tukio la kupanda ndege kutoka jijini Dar es Salaam kwenda Zanzibar bila kujulikana  limeibuka tena, safari hii katika sura mpya kufuatia mtoto huyo kufungua kinywa chake na kuanika mambo ya kichawi, Uwazi lina mkanda mzima.