Jaja Vs Zahir ni shiida, Maximo awaamua mara 3
KWELI Yanga imepania kufanya kweli, kila mchezaji anataka kuonyesha uwezo wa juu, lakini ushindani huo umesababisha upinzani kuwa mkali kwa wachezaji wa timu hiyo, beki Rajab Zahir dhidi ya Genilson Santos ‘Jaja’, ambapo wamekuwa na kazi ya ziada mazoezini.
Jana pia kwenye Viwanja vya Tanganyika
Packers, Kawe jijini, Zahir alipewa jukumu la kumdhibiti Jaja ambapo
shughuli ilikuwa pevu, baada ya muda mambo yakawa kama ya juzi.
Wakiwa katikati ya mazoezi, Zahir alimkwatua Jaja kwenye kifundo cha mguu wa kulia, kitendo kilichosababisha Jaja kukasirika na kumvaa beki huyo, lakini kabla ya kumfanya chochote, Maximo aliingilia na kusimama kati yao kisha kuanza kutoa maelezo kwa wote wawili.
Wakiwa katikati ya mazoezi, Zahir alimkwatua Jaja kwenye kifundo cha mguu wa kulia, kitendo kilichosababisha Jaja kukasirika na kumvaa beki huyo, lakini kabla ya kumfanya chochote, Maximo aliingilia na kusimama kati yao kisha kuanza kutoa maelezo kwa wote wawili.
No comments:
Post a Comment