Friday, 29 August 2014

WAPIGANAJI WA ISIS WATOA ONYO LINGINE KWA MAREKANI


Mateka 15 wa Kikurd wanaoshikiliwa na wapiganaji wa ISIS.

SAA chache baada ya kuuwa wanajeshi 300 wa Syria, Kundi la wapiganaji wa ISIS limetoa onyo lingine kwa Marekani likiachia video inayowaonyesha mateka 15 wa Kikurd ambao nao watauawa iwapo Marekani haitaondoa majeshi yake.



ISIS wamesema wataendelea kuwachinja mateka hao mpaka Marekani itakapoondoa majeshi yake.
Katika video hiyo, Kundi la ISIS linaonekana likimchinja mmoja wa mateka hao wa Kikurd waliokamatwa wakati wa mapigani nchini Iraq.

Wapiganaji wa ISIS wakiwaswaga wanajeshi zaidi ya 200 waliokamatwa katika ngome ya anga ya Tabqa nchini Syria katika jangwa kuelekea eneo la mauaji.

No comments:

Post a Comment