Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakifuatilia mkutano huo.
TAASISI ya Tanzania Kwanza imewapa wajumbe wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) siku saba kurudi bungeni la sivyo itatoa siri ya umoja huo kupokea fedha chafu, kutoka kwa taasisi kubwa ya nje ya nchi, kupitia asasi moja ya kiraia, kwa lengo la kuhakikisha nchi haitawaliki!.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Agustino Matefu wakati akiongea na wanahabari leo katika Ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment